MAGOLI YA BAROTELI YAIPELEKA ITALY KOMBE LA MABARA.


          
Baada ya kikosi cha timu ya taifa ya Italia kuingia fainali ya michuano ya ulaya shirikisho la soka duniani FIFA limetangaza mwaliko rasmi wa timu hiyo kwenye michuano ya mabara kwa mwaka 2013.
Italia ilijitengezea mwaliko huo usiku wa jana baada ya kumuondoa mjerumani kwa idadi ya magoli mawili na kufanikiwa kuingia fainali itakayochezwa jumapili dhidi ya Hispania.
Katika michuano hiyo iliyoanzishwa na FIFA mwaka 1997 Italia in nafasi ya kukataa mwaliko kama ilivyowahi kufanywa  miaka  ya nyuma na nchi za ujerumani na Ufaransa.
Mabingwa mtetezi na mshiriki wa fainali ,Hispania tayari imekata tiketi ya kushiriki michuano itakayofanyika nchini Brazil kutokana na kuwa bingwa mtetezi wa kombe la dunia.

0 comments:

Post a Comment