Tiketi za Simba na Yanga kuanza kuuzwa kesho.



Tiketi kwa ajili ya mechi ya Yanga na Simba itakayochezwa keshokutwa (Oktoba 3 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam zitaanza kuuzwa kesho kwenye katika vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Mechi hiyo namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa moja kamili usiku.

Vituo vitakavyotumia kuuza tiketi hizo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Uwanja wa Taifa, Kituo cha Mafuta OilCom Ubungo, Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio/Samora, Dar Live Mbagala na Kituo cha Mafuta Buguruni n ate=iketi zitaanza kuuzwa saa nne kamili asubuhi.

Kiingilio cha chini kwenye mechi hiyo ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani , wakati shilingi 7,000 itakuwa kwa viti vya Blue.

Lakini Sh. 10,000 ni kwa viti vya rangi ya chungwa huku VIP C itakuwa sh. 15,000. Kwa upande wa VIP B tiketi ni sh. 20,000 na VIP A kiingilio kitakuwa sh. 30,000.

Wakati huo huo, mwamuzi Mathew Akrama kutoka Mwanza ndiye atakayechezesha mechi hiyo. Waamuzi wasaidizi ni Samuel Mpenzu kutoka Arusha na Efrony Ndissa wa Dar es Salaam wakati mwamuzi wa mezani ni Oden Mbaga pia wa Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment