Mbunge wa Iringa mjini kupitia tiketi
ya CCM Viti maalum Mh, Ritta Kabati ameahidi kuchangia kisi cha shilingi laki
mbili za kitanzania kwaajili ua kuisaidia timu ya Basketi mkoa wa Iringa ili
iweze kufanikisha safari yake ya jijini Tanga kwenye michuano ya Taifa cup kwa
mwaka 2012.
Kabati amesema ni muhimu kwa viongozi
wengine kujitolea kusaidia michezo kutokana na nafasi na faida kubwa
inayopatikana kwenye michezo, huku akiongeza kuwa kuinua kikapu nyanda za juu
kusini kunaleta faraja kubwa kwa mpaka sasa ni takribani miaka 15 Iringa haina
cha kujivunia katika michezo takribani yote.
Naye makamu mwenyekiti wa muda wa
shirikisho la kikapu mkoa Iringa IRBF amewataka wadau kuwa na imani katika
kuchangia suala hilo kwa uongozi uliopo madarakani kwa muda huu umetengeza
msisitozo wa hali ya juukatika kurejesha heshima ya mchezo wa kikapu mkoa humo.
Harambee ya hiyo ya kuchangia timu ya
mkoa inaendelea IRBF kwa kushirikiana na kituo cha redio Ebony fm ya mkoani
humo.
0 comments:
Post a Comment