
Timu ya
taifa ya England ya mchezo wa Cricket itaanza mchakato wa kutafuta mdhamini wa
mavazi ya timu hiyo baada ya mdhamini mkuu ambaye ni kampuni ya Blit Insurance kutangaza kutoongeza mkataba
mara baada ya kumalizika.
Katika
mkataba huo uliokuwa ukihusika na utoaji wa vifaa vya mazoezi na mechi
mbalimbali za timu hiyo uliiwezesha England kudumu kwa mafanikio makubwa kwenye
michezo yake ya kimataifa.
Kwa mujibu
wa viongozi wa kampuni hiyo wamesema kuwa wamefikia uamuzi huo baada ya kutosheka
na kazi waliyoifanya na timu hiyo tangu mwaka 2011 na huku ukielezwa kuwa
mkataba huo unamalizika rasmi mapema mwaka 2014.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa bodi
ya biashara ya Cricket katika mataifa ya England na Wales Cricket, John Perera
amesema taratibu za kuvunjwa kwa mkataba huo zitafanyika mapema kama watapa
mrithi wa nafasi hiyo. Kampuni ya Blit iliingia mkataba na England mapema mwezi January mwaka 2011 ikichukua nafasi ya kampuni ya KIA iliyomaliza muda wake. Lakini pia BLIT.
Chanzo ni BBC.
0 comments:
Post a Comment