
Raisi wa TFF Leodga Tenga
Uongozi wa Shirikisho la soka nchini TFF, umesema
kuwa suala la mgogoro wa nembo ya
mdhamni wanaliweka pembeni na kuwaachia wadhamini na vilabu husika wakae
nakujadili suala hilo.
Raisi
wa TFF Leodga Chila
Tenga amesema hayo hii leo katika Mkutano maalum na Waandishi wa Habari,
uliofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam,amesema msimu uliopita Vodacom
walimalizana na Yanga bila ya kuishirikisha TFF, katika mgogoro huo wa nembo.
Kuhusu uchaguzi Tenga amewataka wagombea
kuwasilisha vielelezo vyenye sifa za kugombea na kusoma kanuni za uchaguzi ili
kuondoa migogoro katika chaguzi mbalimbali za vyama vya soka.
Katika mkutano Tenga alimaliza kwa kusema kuwa
uongozi wa Mpira ni wito na si kazi kama wanavyofikiri watu.
0 comments:
Post a Comment