Ligi kuu ya Tanzania bara iliendeleahapo
jana kwa michezo minne kupigwa kwenye viwanja tofauti ambapo kwenye uwanja wa
taifa jijini Dar es salaam, klabu ya soka ya Yanga iliibuka na ushindi wa
magoli 3 kwa 0 dhidi ya vibonde wa ligi hiyo Polisi Morogoro.
Magoli ya Yanga yalifungwa na kinda wa
timu hiyo Simon Msuva, Didier Kavumbagu na Hamisi Kiiza aliengia akitokea
benchi.
Matokeo ya michezo mingine ni Azam FC
hii leo ilishindwa kushika usukani wa ligi kuu bara baada ya kulazimishwa sare
ya goli 1 kwa 1 na maafande wa Ruvu shooting.
Kule Manungu nako mambo yalikuwa magumu
kwa Mtibwa Sugar baada ya kulazimishwa sare ya goli 1 kwa 1 na wakata miwa
wenzao Kagera Sugar.
Kwa upande wa Coastal Union waliokuwa
nyumbani kwao kule mkoani Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani baada ya kuibuka na
ushindi wa goli 1 kwa 0 dhidi ya African Lyon.
.................
Wakati huo huo, tukigeuza jicho katika
ligi daraja kwa mwakilishi wa mkoa wa Iringa timu ya Kurugenzi ya Mufindi ilishindwa
kutamba ikiwa nyumbani kwenye uwanja wa Wambi uliopo mjini Mafinga baada ya
kufungwa goli 1 kwa 0 na Majimaji ya Songea.
Katika uwanja wa Jamhuri pale Morogoro
timu ya Mbeya City iliibuka na ushindi wa goli 1 kwa 0 dhidi ya Burkinafaso
huku goli Mbeya City likifungwa na Fidels Castor katika dakika ya 85 ya mchezo
huo.
Hapo kesho kwenye uwanja wa Jamhuri
mkoani Morogoro timu ya Polisi Iringa itacheza na Mkamba Rangers jioni ya leo
katika kukamilisha ratiba ya raundi ya kwanza.
0 comments:
Post a Comment