FA WAANZA KAZI NA COLE.



 Ashley Cole
                       Cole akiwa na jezi ya England.
Mlinzi wa klabu ya Chelsea na timu ya Taifa ya England Ashley Cole huenda ameingizwa kwenye adhabu na shirikisho la soka nchini England kwa kosa la utovu wa nidhamu.

FA imemuingiza hatia Cole kutokana na kuandika ujumbe wa kuthibisha kuwa aliongopa juu ya utetezi wa tuhuma ya Jonh Terry juu ya ubaguzi wa rangi.

Chama cha soka nchini England FA kimetoa siku tatu kutoka leo ikiwa na maana siku ya Alhamisi Cole awe ameshajibu tuhuma hizo kabla ya mchezo wa kuwania tiketi  ya kombe la dunia dhidi ya San Marino.
Kwa upande wake mshambuliaji wa zamani wa Newcastle united Alan Shearer mwishoni mwa juma lililopita aliitaka FA kumfungia nyota huyo haswa akose mchezo dhini ya San Marino huku akikumbushia kufungiwa kwake baada ya kumkosea Nei Lenon mwaka 1998 katika mchezo wa ligi.

0 comments:

Post a Comment