TASWA YAFIKIA HATUA YA MWISHO YA MKUTANO MKUU WA WAANDISHI WA HABARI



Sekretarieti ya chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA imefikia hatua ya mwisho ya mazungumzo na mdhamini wa Mkutano Mkuu wa chama hicho, unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao katika tarehe ambayo itatangazwa rasmi.
Kamati ya Utendaji ya TASWA ilikubaliana katika kikao chake mwezi uliopita kuwa Mkutano Mkuu wa TASWA mwaka huu uwe wa aina yake kwa kuwawezesha wanachama kukaa pamoja na kubadilishana mawazo huku ikashauri mkutano huo ufanyike nje ya Dar es Salaam kama hali itaruhusu.
Akizungumzia hilo katibu mkuu wa Taswa Amiri Muhando, amesema tayari suala la kutafuta mdhamini limefanyika na mdhamini amepatikana, na wapo kwenye hatua ya mwisho ya mazungumzo kabla ya kutajwa mapema wiki ijayo .
Kwa upande mwingine Muhando amewaka wanachama ambao hawajalipa ada zao wafanye hivyo kwa kuwasiliana na Mhazini wa chama au Mhazini Msaidizi ili waepuke usumbufu wa kushindwa kuhudhuria mkutano huo

0 comments:

Post a Comment