KIM KUFANYA ZIARA VISIWANI ZANZIBAR.



 
                                              Kim Poulsen
Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania(Taifa Stars), Kim Poulsen mwishoni mwa wiki hii ataanza ziara wisiwani Zanzibar kuangalia Ligi Kuu ya nchini humo.

Kim anatarajia kushuhudia takribani mechi tano akianzia kisiwani Pemba ambapo kati ya Oktoba 19 na 21 atashuhudia mechi mbili zitakazochezwa kwenye Uwanja wa Gombani. Mechi hizo ni kati ya mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Super Falcon watakao cheza na vinara wa ligi hiyo Bandari, na baadaye mechi kati ya timu ya Duma na Bandari.

Baadaye atakwenda Unguja kwenye Uwanja wa Amaan ambapo baadhi ya mechi alizopanga kushuhudia ni kati ya Mtende na Chipukizi, Mundu na Jamhuri na KMKM dhidi ya Zimamoto.

Ziara ni moja ya mikakati mikubwa ya kuhakikisha anapata kikosi bora cha timu ya taifa ya Tanzania.

0 comments:

Post a Comment