LIVERPOOL KUKARABATI UWANJA WA ANFIELD



 Anfield
                                 Uwanjwa wa Anfield.
Klabu ya Liverpool, imetangaza mpango wake wa kuboresha  uwanja wake wa Anfield wanao utumia michezo mbalimbali  na kuacha mpango wa kujenga uwanja wa mpya wa timu hiyo.
Mkurugenzi wa Liverpool, Ian Ayre, amethibitisha kuwa uwanja huo utaboreshwa kutoka  mashabiki 45,276 hadi 60,000  na upanuzi huo wa uwanja utagharimu kiasi cha paundi milioni 150.
Amesema uongozi wa Liverpool, umelipa kiasi cha paundi milion 25 kama kodi ya kupata eneo la kutanua uwanja huo, wakati mchoro kamili wa ujenzi huo utawekwa wazi rasmi mwezi ujao huku mpango wa ujenzi rasmi kuanza kazi majira ya kiangazi mwakani.
Mpango huo utajumuisha mitaa kadhaa ambayo itaingizwa katika eneo la uwanja ikiwemo mitaa, Lother,Alroy na Sybil huku maeneo yatakayofanyiwa maboresho makubwa ni eneo la jukwaa kuu na maeneo  baadhi ya maeneo ya muhumi ya klabu hiyo.
Chanzo na BBC.

0 comments:

Post a Comment