
Katibu wa Yanga, Mwalusako
Baada ya kupokea kichapo kwenye mchezo wa ligi hapo
jana dhidi ya Kagera Sugar uongozi wa labu ya Yanga umesema timu yao ilifungwa
kimchezo na si kwa sababu nyinginezo.
Hayo yamesemwa hii leo na katibu wa Yanga Lawrence
Mwalusako kuwa sababu zilizosambazwa kuwa walifikia hoteli mbovu na chakula
kibovu, ndio sababu ya kufungwa siya kweli.
Mwalusako amekanusha habari zilizoandikwa na gazeti
moja la leo, kwamba wachezaji wake walilala wawili wawili kitanda kimoja mjini
Bukoba.
Kuhusu michezo inayofuata Mwalusako amesema kwa
sasa wanatafuta mbinu nzuri za kupata ushindi nje ya Dar es Salaam ambayo
imekuwa kikwazo kwa kiasi kikubwa.
0 comments:
Post a Comment