Uongozi wa chama cha soka wilaya ya Mufindi MUDIFA umevitaka
vilabu vya wilaya hiyo kujiandaa kwa ligi ya wilaya wakati wakisubiri maelezo
ya mfumo mpya wa ligi za wilaya toka
katika shirikisho la soka nchini TFF.
Katibu mkuu wa MUDIFA, Festor Kilipamwambu alizungumza hayo
Sambamba na kuwataka watendaji wa kata takribani zote za wilayani Mufindi
kuandaa viwanja kwaajili ya kuchezewa michezo ya ligi hiyo iliyoshindikana
kuanza mwezi huu.
Kilipamwambu amesema kata zinatakiwa kuandaa viwanja ili
kutimiza hazma ya kuchezwa ligi kwa mtindo wa nyumbani na ugenini sambamba na
kukuza mchezo wa soka wilayani humo.
Kabla ya kuanza kwa ligi ya wilaya tayari timu za Mucoba FC,
Ifwagi, JKT Mafinga na Changarawe zimeshafuzu kucheza ligi ya mkoa kutokana na
mabadiliko ya mfumo katika uendeshaji wa ligi za Tanzania bara.
0 comments:
Post a Comment