NJOMBE MJI KUCHEZA NA MAJIMAJI.



Timu ya Njombe mji, toka mkoa mpya wa Njombe siku ya jumapili itacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Majimaji ya songea kwenye uwanja wa Amani, Mjini Makambako.
Akizungumzia mchezo huo, katibu mkuu wa Njombe Mji, Obeid Mwakasungura amesema mchezo huo ni maandalizi tosha ya ligi ya wilaya kwa mwaka huu.
Amesema tayari mpaka sasa timu hiyo imezidi kuimarika kufuatia michezo waliocheza dhidi ya Mbeya City na Serengeti Boys, ambayo yote walimaliza kwa kufungwa.
Msimu uliopita Njombe mji, ilishindwa kufanya vyema kwenye hatua ya mwisho ya ligi mkoa kutokana na kushindwa kumudu mikiki ya upinzani uliokuwemo toka kwa timu nyingine za mkoa wa Iringa ikiwemo Kurugenzi.

0 comments:

Post a Comment