CARLISLE AIPONDA DHABU YA TERRY



Clarke Carlisle
Mwenyekiti wa chama cha wachezaji wa kulipwa nchini England PFA, Clarke Carlisle amesema kuwa adhabu aliyopewa mlinzi wa Chelsea Jonh Terry kwa kusimamishwa michezo minne haikutosha kama adhabu ya mchezaji huyo.
Carlisle ambaye kwa sasa anacheza klabu ya York City ya nchini humo, amesema kuwa angalia adhabu ya Suarez iliyotolewa 20  Decemba  2011, kwa kosa la u ubaguzi  dhidi ya Patrice Evra alitozwa michezo minane na faini ya paundi 40000 huku akipewa kiasi cha siku 14 za kukata rufaa.
Lakini Terry amefungiwa michezo minne na faini 220000 huku akipewa siku 18 za kukata rufaa yake.
Carlisle amitaka kamati ya nidhamu ya FA kuwa kuongeza adhabu  kwa terry na kumfanya achangie katika kampeni dhidi ya ubaguzi wa rangi.

0 comments:

Post a Comment