KAMWAGA AVIZIBA MDOMO VYOMBO VYA HABARI.



 
                    Msemaji wa Simba E.Kamwaga
Uongozi wa klabu ya Simba umevitaka vyombo vya habari kusema uongo juu ya klabu yao haswa kuhusu wachezaji wa klabu hiyo,
Hayo yamesemwa na msemaji wa timu hiyo Ezekiel Kamwaga mchana wa leo wakati akizungumza kuhusu uzushi wa kusimamishwa kwa Mrisho Ngasa juu ya kucheza chini ya Kiwango dhidi ya Yanga siku ya jumatano.
 Kamwaga amesema kuwa hakuna maamuzi kama hayo ndani ya Simba na sababu ya Ngasa kucheza chini ya Kiwango imetokana na kusumbuliwa na ungonjwa wa Maralia. Huku akithibitisha kuwa nyota huyo hatokuwemo kwenye kikosi cha kesho kitakacho cheza na JKT Orjoro.
Aliongeza kuwa si Ngasa pekee atakae  kosa mchezo ila mlinzi mahiri wa timu hiyo Shomary Kapombe anaeumwa bega na mguu pamoja na Shamte Haruna alieumia akiwa mazoezini visiwani Zanzibar.
Kwa upande wa malalamiko ya Mapato katika mchezo wake dhidi ya Yanga Kamwaga amesema kwa upande wao hawakuona mapungufu na kuwataka wadau wajitokeze katika michezo ili kuongeza kipato zaidi , ila amevitaka vilabu vyote kuwa na miradi yenye kuchangia maendeleo ya vilabu hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment