RITTA KABATI ATEKELEZA AHADI YA KIKAPU.



                 
                                       Ritta Kabati
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia tiketi ya chama cha mapindui mheshimiwa Ritta Kabati hapo jana amekabidhi  kiasi cha shilingi laki mbili kwa chama cha mpira wa kikapu mkoani Iringa ambayo kwa sasa inaiandaa timu ya mkoa inayotarajiwa kushiriki michuano ya taifa Cup  itakayofanyika jijini Tanga mwezi huu.
Akizungumza na Twalib Omary mara baada ya kutoa pesa hizo Kabati amesema kuwa hiyo ilikuwa ni sehemu ya ahadi aliyotoka katika kipindi chote cha mapumziko ya vikao vya bunge na anatambua umuhimu wa michezo sambamba na mchezo huo wa kikapu ambao umepoteza njia mkoani Iringa.
Aliongeza kwa kuwataka wadau kujitokeza vya kutosha katika kuisaidi michezo ili kupata timu mahiri zitakazo tuwakilisha katika mashindano mbalimbali hapa nchini,
 Kwa upande wake katibu mkuu wa muda wa chama cha kikapu mkoani iringa IRBF, Jamal Asedi ameshukuru kupokea kiasi hicho na kuwataka wadau wajitokeze kutoa zaidi ili kuhakikisha timu inasafiri, lakini pia amefanunua kuwa michuano hiyo kwa sasa itaanza rasmi Oktoba 29 mwaka huu baada ya 18 iliyopangwa hapo awali.

0 comments:

Post a Comment