Kikosi cha Serengeti Boys
Timu ya taifa ya vijana wenye umri
chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) imefuzu kucheza raundi ya tatu na ya mwisho
kwenye michuano ya kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Vijana
baada ya Misri kujitoa.
Akithibitisha hilo msemaji wa TFF,
Boniface Wambura amesema Serengeti Boys ilikuwa icheze raundi ya pili dhidi ya
Misri Oktoba 14 mwaka huu jijini Dar es Salaamkabla ya kurudiana baada wiki
mbili lakini imeshindikana kutokana na kutokamilika kwa maandalizi ya timu ya
Misri.
Amesema Serengeti Boys itacheza raundi ya tatu kwa kumkabili mshindi
wa mechi kati ya Zimbabwe na Congo Brazzaville. Mechi ya kwanza itachezwa
Novemba 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati ya marudiano itafanyika
ugenini wiki mbili baadaye.
Katika raundi ya kwanza Serengeti Boys
inayofundishwa na Jakob Michelsen kutoka Denmark ilikuwa icheze na Kenya mwezi
uliopita, lakini nchi hiyo ilijitoa katika michuano hiyo ambayo fainali zake
zitachezwa Machi mwakani nchini Morocco.
Zimbabwe na Congo Brazzaville
zitapambana zitapambana kati ya Oktoba 12-14 mwaka huu, Zimbabwe ikiwa mwenyeji
wa mechi ya kwanza wakati ya marudiano itafanyika kati ya Oktoba 26-28 mwaka
huu.
0 comments:
Post a Comment