
Mbunge wa jimbo la IringaMjini kupitia tiketi ya Chadema, Mchungaji Piter
Msingwa, yupo katika mikakati ya kudhamini ligi ya wilaya ya Iringa mjini kwa
msimu wa mwaka 2012.
Akizungumza na Mwananchi mratibu wa michezo katika ofisi ya
mbunge huyo Abu Changawa amesema kuwa udhamini huo utazingatia uandaaji wa timu
zitakazo shirki katika ligi wilaya hiyo, kwa kutoa vifaa vya michezo ikiwemo
jezi na mipira sambamba na posho kwa waamuzi wa michezo ya ligi hiyo.
Aliongeza kuwa lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha soka la
Iringa linarejea katika heshima yake iliyopotea takribani miaka 11 iliyopita.
Majeki amesema,Mh Msigwa bado yupo katika harakati za mwisho ili kufaninikisha zoezi
hilo linalotaka kufanyika kwa mkataba wa mwaka mmoja kati yak e na chama cha
soka wilaya IMDFA.
Msimu uliomalizika wa mwaka 2011 mbunge huyo aliahidi kutoa
zawadi kwa mshindi wa kwanza wa ligi hiyo ambaye ni Magorofani hatimaye
hakuitekeleza ahadi ya zawadi ya jezi.
Lakini pia ahadi hiyo ilitolewa na Meya wa Manispaa ya Iringa
Amani Mwamwindi na katibu wa soka Iringa Eliud Mvela lakini hawakutekeleza
zawadi hizo za washindi wa ligi ya wilaya Iringa
Wakati huohuo katibu msaidizi wa chama cha soka wilaya ya
Iringa mjini, Rashidi Ali Shungu, amesema ligi ya wilaya hiyo itaanza tarehe 10
oktoba na ratiba itatolewa oktoba saba mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment