MALANGALILA KUZIKWA KESHO.



 Benito Malangalila katikati akiwa na katika harakati za Muungano cup
Mazishi ya aliekuwa mbunge wa jimbo la Mufindi Kusini muheshimiwa Benito Malangalila yaliyopangwa kufanyika leo yamesogezwa mbele hadi hapo kesho saa 6 kamili mchana.
Akizungumza nasi mratibuwa michuano ya Muungano na mjumbe wa soka la vijana TFF amesema kuwa mazishi ya mwenyekiti huyo wa kamati  ya Muungano yameshindikana kufanyika hivi leo kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya maandalizi ya mazishi hayo.
Lakini mbali na hayo amethibitisha kuwa mpaka itakapofika  usiku wa hii leo kila kitu kitakuwa kimekwenda sawa kwa upande wa maandalizi.
Yasini amesema mpaka leo hii wadau na viongozi mbalimbali wamekuwa wakituma salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu Malangalila iliyopo Changarawe mjini Mafinga.
Mung u aiweke  roho ya Marehemu Malangalila mahala pema peponi Amen.

0 comments:

Post a Comment