CHEKA KUPATA PAMBANO LA KULIPWA.



Baada promota maarufu wa ngumi za kulipwa kutoka nchini Misri Richard  Nwoba wa kampuni ya “Louaa Boxing Promotions” kuzitembelea ofisi za IBF zilizoko jijini Dar-Es-Salaam ili kuona namna ya kupromoti mapambano ya ngumi katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

Rais wa IBF Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba ya Uarabu na Uajemi “Onesmo Ngowi katika ziara hiyo ya Nwoba wamefikia makubaliano ya kushirikiana na makampuni matatu ya Tanzania kupromoti mapambano manne ya ubingwa wa IBF katika mwezi wa Novemba.

Katika makubaliano hayo mabondia kadhaa wa Tanzania, Kenya na Misri watapambana kuwania mataji manne ya IBF Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba za Uarabu na Uajemi. huku ikiwa faraja kwa bondia Francis Cheka wa Tanzania ambaye atachuana bondia toka nchini Oman, Amin Saad Mabrook katika mpambano utakaofanyika mwezi Novemba mwaka huu.

Richard Nwoba ni bondia wa zamani na makao yake makuu yako katika jiji la Cairo nchni Misri ambako anaendesha biashara ya ulinzi wa makampuni pamoja na kupromoti ngumi za kulipwa akiendesha kampuni ya “Louaa Boxing Promotions.
MWISH

0 comments:

Post a Comment