HII NDIO RATIBA YA LIGI DARAJA KWANZA KWA MICHEZO YA KESHO.



Kwa upande wa kundi A, ligi hiyo inaendelea hapo kesho timu ya Polisi Iringa kucheza Mbeya City (Samora, Iringa), Majimaji vs Small Kids (Majimaji, Songea), Burkina Faso vs Mkamba Rangers (Jamhuri, Morogoro) na Kurugenzi Mufindi vs Mlale JKT (Wambi, Mufindi).
  
Kwa upande wa kundi B, hapo kesho Ndanda FC vs Green Warriors (Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Tessema (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 28 mwaka huu ni Ashanti United vs Transit Camp (Mabatini, Pwani) na Oktoba 29 mwaka huu ni Moro United vs Polisi Dar es Salaam (Chamazi, Dar es Salaam).

Raundi ya pili kwa upande wa kundi C, hapo kesho,Polisi Tabora vs Polisi Dodoma (Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mwadui vs Polisi Mara (Kambarage, Shinyanga), Kanembwa FC vs Morani (Lake Tanganyika, Kigoma) na Pamba vs Rhino Rangers (Kirumba, Mwanza).

0 comments:

Post a Comment