ROONY KUWA NAHODHA SIKU YA JUMAMOSI.



            Wayne Rooney
Kiungo wa timu ya taifa ya Englanda Frank Lampard ameondolewa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya England baada ya kupata jeraha la goti wakati akiwa katika mazoezi na timu hiyo.
Chama cha soka cha England FA kimesema kuwa  kiungo huyo atarejea katika timu ya Chelsea kwaajili ya matibabu kabla jumapili kujiunga tena na kikosi cha England kwajili ya mchezo dhidi ya Poland utakaocheza siku ya jumanee.
Kutokana na hali hiyo kocha Roy Hogson amefanya maamuzi ya kumwita mchzaji wa Liverpool,Jonjo Shelvey  kwaajili kuziba nafasi hiyo na mlinzi wa Chelsea Ryan Bertrand anaeziba nafasi ya beki wa Arsena Kieran Gibbs ambaye pia ni majeruhi.
Siku ya Ijumaa England inakabiliwa na mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia za mwaka 2014 kule nchini Brazil dhidi ya San Marino kabla ya kuwakabili Poland siku ya Jumanne.
Wakati huo mshambuliaji wa Manchester united, Wayne Rooney ametajwa kuwa atavaa kitambaa katika mchezo wa Ijumaa dhidi ya San Marino utakaoshuhudiwa na washabiki wapatao  90,000  kwenye uwanja wa Wimbley.
Roony mwenye umri wa miaka 26 na kucheza michezo 76, anachukua nafasi hiyo badala ya nahodha wa England na Frank Lampard kuondolewa kwenye orodha  ya wachezaji watakaoshiriki siku hiyo kutokana na majeruhi.
Kikosi cha England cha sasa makipa ni Fraser Forster (Celtic), Joe Hart (Manchester City), John Ruddy (Norwich)
Walinzi Leighton Baines (Everton), Ryan Bertrand (Chelsea), Gary Cahill (Chelsea), Ashley Cole (Chelsea), Phil Jagielka (Everton), Glen Johnson (Liverpool), Joleon Lescott (Manchester City), Ryan Shawcross (Stoke), Kyle Walker (Tottenham)
viungo Michael Carrick (Manchester United), Tom Cleverley (Manchester United), Steven Gerrard (Liverpool), Adam Johnson (Sunderland), Aaron Lennon (Tottenham), James Milner (Manchester City), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Jonjo Shelvey (Liverpool), Theo Walcott (Arsenal)
washambuliaji ni Andy Carroll (West Ham), Jermain Defoe (Tottenham), Wayne Rooney (Manchester United), Danny Welbeck (Manchester United)

0 comments:

Post a Comment