
Aliekuwa kocha wa Bolton, Owen Coyle
Kocha wa klabu ya Bolton Wonderers, Owen Coyle amefukuzwa
kazi katika klabu hiyo aliyokuwa akiifundisha tangu tangu alipojiunga nayo January
8 mwaka 2010.
Kocha huyo ambaye katika miaka ya 90, aliwahi kuchezea timu
hiyo, kufutwa kwa mkataba wake kumetokana na kushinda mechi tatu kati ya kumi za
ligi ya mabingwa ya nchini England huku ikiwa nafasi ya 18 kwenye msimamo wa
ligi hiyo.
Baada ya maamuzi hayo mwenyekiti wa Bolton Wonderers, Phil
Gartside, ameushukuru mchango wa Coyle na jopo lake katika kipindi chote
alichokuwa na timu hiyo.
Kwa upande wake Coyle, amesema alijitahidi kufuata vile
Bolton inataka tangu akiwa mchezaji lakini mambo yamekuwa magumu kwa hiyo hana
budi kuwashukuru viongozi na mashabiki wa klabu hiyo.
Coyle mwenye umri wa miaka 46, aliwahi kuifundisha timu ya
Burnley kwa miaka mitatu na kuipandisha ligi kuu ya England EPL kabla ya kuhama
na kujiunga na Bolton Janury 8 2010
ambayo alishuka nayo msimu wa 2011-2012.
0 comments:
Post a Comment