
Zlatani akiwa na jezi PSG.
Baada ya sare ya jana dhidi ya Olimpic
Marsele kocha wa Paris Saint-Germain Carlo Ancelotti amesema kuwa hakuvutiwa na
kiwango cha mshambuliaji wake Zlatan Ibrahomovic katika mchezo huo wa saba wa
Ligi one.
katika mchezo huo Zlatan alifunga
magoli mawili na kusababisha matokeo hayo suluhu lakini kocha huyo wa kitaliano
amesema anaujua vizuri uwezo wa Zlatan kuliko alivyofanya kazi kwenye mchezo
huo wa ligi.
Mashabiki waliowengi wa PSG wanadai
kuwa mshambuliaji amechoka kutokana na kutumika katika michezo iliyopita kitu
ambacho Ancelot anadai kuwa na imani ya nyota huyo alikuwa fiti kwa asilimia 80
za kucheza vizuri.
Tangu ajiunge na PSG Zlatan mwenye umri
wa miaka 31 anaongoza kwa magoli kwa kufunga magoli 9 katika michezo nane ya
ligi nchini ufaransa sambamba na goli moja la ligi ya mabingwa barani ulaya
alilofunga katika mchezo dhidi ya
Dyanamo Kiev.
0 comments:
Post a Comment