MWALIMU WA KLITSCHKO AFARIKI DUNIA.



 Emanuel Steward
                        Steward wakati wa uhai wake.
Mwalimu mkongwe wa mchezo wa ngumi, Emanuel Steward wa marekani,amefariki dunia mchana wa jana akiwa hospitalini jijini Chicago nchini humo.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, raisi wa shirikisho la ngumi za nchiniMarekani HBO, Ken Herishman amesema kifo hicho kimetokea wiki kadhaa baada ya kocha huyo kulazwa hospitali kwaajili ya kufanyiwa upasuaji wa ugonjwa wa kansa.
Steward amefariki akiwa na umri wa mia 68 huku akiwa na rekodi ya kuwafundisha mabondia mbalimbali ulimwenguni wakiwemo Wilfred Benitez, Julio Cesar Chavez, Oscar de la Hoya, Evander Holyfield, Mike McCallum and James Toney.
Mpaka anakutwa na mauti Steward alikuwa ndiye kocha mkuu wa bondia wa Ukraine Vladmil Klitschko ambaye kwa sasa anatikisa ulimwengu kwa ubora wa mchezo huo.
Katika kupokea msiba huo mzito Klitscho amesema kifo cha Steward ni pigo kwake huku akikiri kuishi naye kwa mafanikio na marehemu alikua akiipenda kazi ya Vladmir kutokana na jinsi anavyojituma katika mechi zake.
Katika kipindi chake cha ubondia Steward mwaka 1980 alikuwa bingwa dunia baada ya kumpokonya ubingwa huo Hilmer Henky aliekuwa akitamba kipindi hicho na hadi anafariki Stewarda ameacha kitengo cha mazoezi ya ngumi kinacho julikana kwa jina la Kronky Gym iliyopo jijini Detrot nchini Marekani.

0 comments:

Post a Comment