BONGO TUNASUASUA FA WAMEAMUA.



          
                                 St Gerge`s Park
Chama cha soka cha nchini England FA, kimefungua kituo cha kukuza na maendeleo ya soka nchini humo kinachojulikana ka St George`s Park Complex.
Mwenyekiti wa FA David Bernestein amesema kituo hicho chenye upana wa ekali 330, na kimegharimu kiasi cha paundi milioni 105 katika kukamilisha ujezi wake kule jijini Stafford shire.
Amesema lengo ni kuwa na wachezaji wengi wa kimataifa na wenye viwango bora ndio maana wameweka mafunzo ya ukocha, madawa pamoja saikolijia ya michezo katika kituo hicho.
Timu ya taifa ya England inayojiandaa kucheza na San Marino katika mchakato wa kutafuta tiketi ya kombe la dunia wiki hii itakuwa ya kwanza kufanya maandalizi kwenye kituo hicho kipya cha soka

0 comments:

Post a Comment