COLE ASAMEHEWA NA FA.



              
                    Mwenyekiti  waa FA,David Bernstein
Mlinzi wa klabu ya  Chelsea na Ashley Cole, amefutiwa adhabu ya kufungiwa kuchezea timu ya taifa baada ya kuomba radhi kutokana na kauli aliyo itoa hivi karibuni katika mtandao wa kijamii.
Mwenyekiti wa  chama cha soka nchini England FA, David Bernstein amesema, usiku wa jana Cole ameomba radhi juu ya kosa la utovu wa nidhamu alilolifanya.
Amesema kutoka na maamuzi hayo aliyoyafanya Cole yupo huru kulitumikia taifa lake huku kukiwa na uwezekano wa kuwemo kwenye kikosi cha kwanza kitakacho anza dhidi ya San Marino siku ya Ijumaa.
Juma lililopita Cole aliandika maneno ya kejeli kwenye mtandao wa kijamii unaojulikana kama Twitter, kwamba FA wamefanya vizuri na ushahidi wake ulikuwa wa uongo juu ya tuhuma za ubaguzi wa rangi zinazo mkabili, Jonh Terry.

0 comments:

Post a Comment