WAGOMBE WA TEFA WAPATIKANA.



Wagombea 13 kati ya 15 waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) wamepitishwa baada ya usaili uliofanyika juzi katika ofisi za TFF.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, amesema waliopitishwa kwenye nafasi ya uenyekiti ni Isabellah Kapera, Joan Minja na Lina Kessy.

Makamu Mwenyekiti ni Rose Kisiwa wakati wanaowania nafasi ya Katibu Mkuu ni Amina Karuma na Cecilia Makafu. Mgombea pekee wa nafasi ya Katibu Msaidizi, Macky Mhango wakati nafasi ya Mhazini ampepita Rose  Msamila.

Furaha Francis na Zena Chande watawania nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa (TFF) wakati waliopita nafasi za ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TWFA ni Triphonia Ludovick Temba, Rahim Maguza na Sophia Charles.

Mchakato wa uchaguzi wa TWFA uko katika kusikiliza rufani zitakazo anzia Oktoba 15-17 mwaka huu. Rufani zinatakiwa zifike kwa Katibu Mkuu wa TFF kabla ya saa 10 kamili jioni ya Oktoba 17 mwaka huu.

Uchaguzi unatarajiwa kufanyika Novemba 4 mwaka huu ni Julliet Mndeme na Jasmin Soud walioomba ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF. Wagombea hao ambao pia walikuwa wamewekewa pingamizi hawakufika kwenye usaili.
Chanzo TFF makao makuu.

0 comments:

Post a Comment