
Hali ilivyokuwa jana.
Shirikisho la
soka nchini Poland, PFA, limesema kuwa linaweza kufidia tiketi za mashabiki
walioingia katika uwanjani kushuhudia mchezo kufuzu fainali za kombe la dunia, kati
ya Poland na England ambao haukucheza usiku wa jana.
Washabiki
takribani 2500 wa kingereza walisafiri kwaajili kushuhudia mechi hiyo
iliyoahirishwa kutokana na uwanja kujaa maji, tayari PFA wamethibitisha kuwa
wanafahamu kiasi cha tiketi zilizo nunuliwa na zilizo tumika na watarejesha
tiketi kwa wale mashabiki walioingia
uwanjani hapo jana.
Kwa upande wake mkurungezi wa England, Adrian Bevington amesema kufidia
kwa tiketi za washabiki ndicho wanachotarajia lakini hawawezi kutoa maamuzi
yoyote juu ya suala hilo kwa kuheshimu majukumu ya kiutawala.
Hapo jana
mchezo kati ya England na Poland ulivunjika baada ya kunyesha kwa mvua
kubwa iliyopelekea kufutwa kwa mchezo
uliopangwa kufanyika kwenye uwanja wa Warsaw nchini Poland.

hii ilikuwa michuano ya ulaua France na Ukraine juni 15-2012 pale Dombas nchini Ukraine mechi ilisogezwa mbele.
0 comments:
Post a Comment