HALI ILIVYO KWENYE MAZISHI YA VICK MACHA.




 Vick Macha enzi  za uhai  wake akiwa katika hifadhi Taifa Ruaha wakati wa ziara ya wanahabari Iringa kuhamasisha utalii wa ndani kwa watanzania
Mwandishi wa habari wa Nipashe Iringa VickyMacha  Kushoto enzi za uhai wake akipata maelezo kutoka kwa mtaalam wa hifadhi Bw Marando

Marehemu Vicky Macha kulia akiwa katika  mkutano wake wa mwisho wa umoja wa vilabu vya  waandishi wa habari nchini Tanzania (UTPC) ambapo pia alikabidhiwa michango ya rambi rambi ya kifo cha Daudi Mwangosi .

Marehemu Vicky Macha  ambaye amefariki asubuhi ya leo katika Hospitali ya mkoa wa Iringa  alizaliwa tarehe 14 /2/1972 mwili  wake utaagwa kesho  katika  katika Hospitali ya mkoa  wa Iringa na msiba kwa  sasa upo eneo ya Kibwabwa Shapria   kata ya Kitwiru katika Manispaa ya Iringa ambako alikuwa akiishi

Zoezi la kuaga mwili litaanza saa 6 mchana kabla ya  kuondoka majira ya saa 8 mchana kuelekea Mjini Moshi mkoani Kilimanjaro kwa Mazishi .

Zoezi la kuaga mwili wa marehemu  litaanza majira ya saa 6 mchana  ili  kuwawezesha wale  waliopo katika msafara kuanza safari mapema kwa mujibu wa marehemu Vicky Bw Philimon Shirima ambaye amezungumza na mtandao huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com jioni  hii kuwa .

Mwanahabari  Vicky Macha ameacha  watoto wawili   huku mtoto mmoja  wa kike akiwa na miaka 16 na wa kiume akiwa na miaka  7.

Tasnia ya habari mkoa wa Iringa na Tanzania kwa ujumla   imepata  pigo  kubwa kwa  kuondokewa na mwanahabari Vicky Macha ambaye alikuwa akiandikia gazeti la Nipashe mkoa wa Iringa na pia alikuwa ni mweka hazina  wa klabu ya  waandishi  wa habari mkoa  wa Iringa (IPC) .

Vicky Macha atakumbukwa kwa jitihada zake mbali mbali alizozifanya katika kudumisha IPC na tasnia ya habari kwa ujumla hata kupendwa na kila mdau wa habari kwa kazi  zake .

Mtandao huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com  pamoja na kuwa msiba huu ni mkubwa zaidi kutokana na Vicky Macha kuwa ni kiongozi mwenzangu ila bado naweza kusema kila nasi itaonja mauti Vicky Ametangulia kuandaa makao ni zamu ya nani ni mwenyezi Mungu anajua hivyo tukeshe  tukiomba maana  hatujui siku  wala saa ya kuianza sasfari kwenda kuanza makao mapya.

JINA LAKE BWANA NA LIHIMIDIWE DAIMA
TAARIFA HII IMETOKA KWENYE MTANDAO WA FRANCIS GODWIN.

0 comments:

Post a Comment