Mch. Msigwa akiwa katika moja harakati za michezo
Uongozi wa
chama cha soka wilaya ya Iringa mjini umemtangaza aliekuwa katibu mkuu wa TFF
Fredirick Mwakalebela, kuwa mdhamini mkuu wa ligi ya wilaya hiyo inayotaraji
kuanza mapema mwezi huu.
Akizungumza
na Blog hii, katibu mkuu wa chama soka wilayani humo IMDFA, Bakari Kamtande
amesema udhamini wa Mwakalebelela umepitishwa kufuatia makubaliano ya vipengele
vilivyopo kwenye mkataba wao wa ligi hiyo.
Amesema
Mwakalebela alikubaliana na vipengele vyote vya mkataba huo sambamba na kutaka
kudhamini ligi hiyo kwa miaka mitatu kitu ambacho FA wilaya ilikataa na
kumpatia miaka miwili pekee ya kudhamini ligi hiyo.

Mwakalebela
Kwa upande
mwingine Kamtande amesema kuwa amesikitishwa na kauli za mbunge wa jimbo la
Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa juu ya kukilalamikia chama cha soka juu ya
kuitengua dhamira yake kudhamini ligi hiyo, amesema Mch. Msigwa alitamka maneno
ya kukidharirisha chama cha soka katika mkutano wa hadhara kuwa IMDFA imeingiza siasa na mianya ya rushwa
kwenye mchezo wa mpira wa miguu wilaya Iringa.
Akitoa ufafanuzi
wa mkataba wake kati ya IMDFA na Msigwa, Kamtande amesema kuwa walitoa nafasi
kwa mbunge huyo kudhamini ligi ila alikataa kukubali baadhi ya vipengele vya
mkataba kiasi ambacho kilipelekea maamuzi ya chama kumkabidhi nafasi hiyo Mwakalebela
aliekubali vipengele vyote sanjari na kudai mkataba wa miaka mitatu ila chama
kilibariki kumpa mkataba wa miaka miwili pekee kwa mitatu ni mingi zaidi.
Aliongeza
Kamtande kuwa anaheshimu mchango wa mbunge huyo katika soka la Iringa ila
anaiondoa heshima yake kutokana na uwajibikaji mbovu wa waratibu wa mbunge huyo
akiwemo Abu Changawa ambaye hivi karibuni TFF iliitaka IRFA kumchukulia hatua
kwa kosa la kufanya vurugu kwenye uchaguzi wa chama cha soka mkoa .
Mwishoni
mwa jumalililopita Mch. Msigwa aliwatangazia wananchi kwenye mkutano wa hadhara
kuwa mianya ya rushwa na siasa iliyoingizwa kwenye soka imemnyima nafasi ya
kukuza soka la Iringa huku akionesha hadharani vifaa vichezo ikiwemo Jezi na
mipira ambavyo alipanga kutoa kwa vilabu kama sehemu ya udhamini wa ligi hiyo.
Nilivyozungumza
naye kwa njia ya simu, Fredirick Mwakalebela, alikubali kuwa ameombwa kudhamini
ligi ila bado hajatoa maamuzi juu kusaini mkataba na hajajua kama kuna mvutano
kati ya chama na Mch Msigwa.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment