LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA OKTOBA 20



                                
Ligi daraja la kwanza Tanzania bara itaanza kuchezwa rasmi Oktoba 20 mwaka huu kwa mgawanyo wa makundi matatu yenye timu nane nane kwa kila kundi moja

Akizungumzia hilo msemaji wa TFF Boniface Wambura amesema uamuzi huo umetokana na kikao cha kamati ya ligi kilichoketi jana jiji Dar es Salaam na kupanga tarehe hio sambamba na kuvitaka vilabu kulipa ada ya ushiriki ambayo ni shilingi laki mbili kabla ya Oktoba 13 mwaka huu.

Amesema ligi hiyo itachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini kwa timu zote 24, na bingwa wa kila kundi atapata nafasi ya kupanda ligi kuu msimu ujao
  
Katika ligi hiyo kundi A lina timu za Burkina Moro, Kurugenzi, Majimaji, Mbeya City, Mlale JKT, Mkamba Rangers, Polisi Iringa na Small Kids ya Rukwa, wakati kundi B linaundwa na Ndanda FC, Ashanti United, Green Warriors, Moro United, Polisi, Tessema, Transit Camp na Villa Squad zote za Dar es Salaam

Kwa upande wa kundi C ni Kanembwa JKT ya Kigoma, Morani ya Manyara, Mwadui ya Shinyanga, Pamba ya Mwanza Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora na Rhino Rangers ya Tabora.

0 comments:

Post a Comment