Jeshi la polisi la nchini Serbia limewatia hatiani watu 12
wakiwemo wachezaji wawili wa timu ya taifa ya England chini ya umri wa miaka 21
kwa tuhuma kusababisha vurugu kwenye mchezo kati ya England na Serbia wakufuzu
fainali za ulaya mwaka 2013.
Jeshi hilo
halikuweka bayana majina ya watu hao ila imeeleza kuwa katika orodha hiyo wamo
wachezaji watano wa timu ya Serbia, makocha wa wasaidizi wa timu zote mbili
sambamba na wachezaji wawili wa England.Kwa upande mwingine jeshi limesisistiza kuwa walioingizwa katika kesi hiyo ya jinai ndio walio thibitishwa na kuanzisha vurugu kutokana na uchunguzi uliofanywa na polisi wa jiji la Krusevac kwa muda wa wiki mbili
Kwa upande wa chama cha soka cha nchini England FA, kimesema kuwa mpaka sasa hawajapokea maelezo yoyote juu ya kesi hiyo na kwasasa wanasubiri maelezo kamili ili waweze kutoa tamko.
Katika mchezo huo wa kuwania tiketi ya michuano ya ulaya ya mwaka 2013 uliochezwa jijini Krusevac nchini Serbia, Octoba 16 mwaka England iliifunga Serbia magoli 1kwa 0