LIPULI YAMTAJA LULANGA KUWA KOCHA WA KLABU HIYO.



Uongozi wa timu ya Lipuli ya mkoani Iringa mwisho umetangaza kamati itakayosimamia masuala ya usajili na ufundi katika klabu hiyo kongwe ya mkoani Iringa,
Akizungumza na mwananchi mwenyekiti wa klabu hiyo iliyobeba jina lenye maana ya Ngome ya Mkwawa Abnery Mrema amemtaja ndugu Pascal Bella kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo huku Ahmadi Lulanga akiwa makamu mwenyekiti wakati katibu mkuu akiteuliwa aliekuwa katibu wa Polisi Iringa msimu uliopita Willy Chikweo.
Kwa upande wa wajumbe wa kamati hiyo ni Edna Kajiba ambaye pia ni katibu wa Netball mkoani iringa, Mheshimiwa Mbata, Mengi Kifyoga pamoja na Benson Massiagi.
Katika taarifa yake hiyo Mrema aliongeza kwa kumtaja Ahmadi Lulanga kuwa kocha wa Lipuli, Pascal Bela kuwa mkurugenzi wa Ufundi na Agustino Msigwa kuwa msemaji wa timu wa timu hiyo.
Mrema amemaliza kwa kusema kuwa uteuzi huo umezingatia maamuzi ya kikao kilichofanyika Desemba 30 kujadili maendeleo ya klabu ya Lipuli huku wakiwa na mikakati mizito ya kuhakikisha hadi kufikia mwishoni mwaka 2013 wawe na uhakika wa kurejea kwenye ligi kuu ya Tanzania bara kuwa mwaka 2015.
Kwa sasa Lipuli ya Iringa inakabiliwa na kibarua kigumu cha kusaka ubingwa wa ligi ya mkoani wa Iringa walioupoteza kwa rufaa ya njombe mji mwaka 2010.

0 comments:

Post a Comment