Meneja wa timu ya Arsenal, Arsene
Wenger, amesisitiza kukamilisha usajili wa nyongeza kwa mshambuliaji wake Theo
Walcott kabla ya kufungwa dirisha dogo la usajili linalo endelea kufanya kazi
hadi mwishoni mwa mwezi huu.
Wenger amesema kwa
uzoefu wake wa kufanya mazungumzo anasilimia 99 mpaka sasa za kumalizaa vizuri
na mshambuliaji huyo huku akisisitiza kuwa huenda mwishoni mwaka wiki hii
usajili wake utaambatana na mchezo wa ligi dhidi ya Chelsea.
Moja kati ya vigezo
vya Walcot mwenye umri wa miaka 23 kutaka kuongeza mkataba ni kupewa nafasi
kama mshambuliaji wa mwisho na kulipwa kiasi cha mshahara wa paundi kali moja kwa wiki.
Lakini Wenger
aliyevuma kutaka kuwasajili Wilfred Zaha wa Crystal Palace na Edinson Cavani wa
Napoli ili kuziba pengo la mchezaji huyo wa kiingereza hakusita kuelezea
dhamira ya kumuacha mchezaji huyo aondoke kama mchezaji huru endapo hatokubali
mkataba mpya.
0 comments:
Post a Comment