Chama cha makocha
mkoa wa Morogoro(TAFCA) kinatarajia kutumia kamati ya uchaguzi ya chama
cha soka mkoa wa Morogoro (MRFA) kusimamia uchaguzi wake baada ya
kukamilisha rasimu ya katiba inayolingana na ile ya chama hicho taifa.
Katibu wa TAFCA Morogoro Edward Hizza
alisema kuwa chama hicho kimeshakamilisha rasimu hiyo ya katiba lakini
kutokana na kukosa kamati ya kusimamia uchaguzi wake. wamelazimika kuitumia
kamati ya uchaguzi ya MRFA ili kuweza kusimamia uchaguzi huo.
Hata hivyo alisema kuhusu viongozi
waliopo madarakani kama watagombea au vinginevyo, hawawezi kulizungumzia kwa
sasa, ingawa akakiri muda wao wa miaka minne wa kukaa madarakani kuwa
ulishamalizika huku baadhi ya waliokuwa viongozi wakiwa wamepoteza maisha.
Nafasi zitakazo waniwa kwenye uchaguzi
huo ambao mpaka sasa haujapangiwa Tarehe, ni mwenyekiti, Makamu
mwenyekiti,katibu mkuu, katibu msaidizi , mweka hazina na msaidizi wake
pamoja na wajumbe wa mkutano mkuu wa mkoa.
0 comments:
Post a Comment