AZAM KUMALIZA NA KCB KABLA YA KURUDI BONGO




Timu ya Azam FC kesho Jumanne itamalizia ziara yake ya mechi za kirafiki jijini Nairobi kwa kucheza dhidi ya K.C.B kwenye Uwanja wa City.
Kikosi cha Azam FC kipo jijini Nairobi kwa ziara ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara pamoja na michuano ya kombe la Shirikisho Afrika, tayari kimeshacheza miwiwli ya kitaifa ya kirafiki dhidi ya AFC Leopards na kufungwa mabao 2 -1 mawili kisha wakachomoza na ushindi wa bao moja kwa sifuri dhidi ya  Sofapaka FC.

 
Kikosi cha Azam FC kinatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam siku ya jumatano, baada ya mchezo wa kesho dhidi ya KCB na kusubiri michezo ya ligi kuu ya Tanzania bara raundi ya pili.
Naye Kocha Stewart Jahn Hall amesema wachezaji wote wako safi kwa mchezo huo dhidi ya KCB  utakao chezwa kesho kwenye uwanja wa City wenye nyasi bandia sawa na uwanja wao wa chamazi.


Wakati Azam wakitarajiwa kurejea nyumbani siku ya jumatano kwa ajili ya kusubiri mzunguuko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, kamati ya ligi ya shirikisho al soka nchini TFF inasubiriwa kutoa kauli ya kuendelea kwa ligi hiyo kama ilivyopangwa, ama kusogeza mbele tarehe.

Afisa habari wa TFF Bonifas Wambura amesema kamati ya ligi inasubiriwa kufanya hivyo, kufuatia sakata la mamlaka ya mapato nchini TRA kuchukua sehemu ya fedha za maandalizi za vilabu vya ligi kuu, kutokana na deni la kodi ambayo ilistakiwa kupitia mishahara ya makocha wa timu za taifa.

Bonifas Wambura amesema licha ya kauli ya kuanza kwa mzunguuko wa pili kusubiriwa, pia kamati ya ligi inasubiriwa kutoa kauli ya kuendelea kwa liugi daraja la kwanza ambayo nayo ilisimama.


0 comments:

Post a Comment