
Zikiwa zimesalia siku chache kabla ya
fainali za kombe la mataifa ya Afrika kuanza nchini Afrika kusini kocha wa timu
ya taifa ya Ghana Kwesi Appiah amemuondoa kikosini mchezaji Andre ‘Dede’ Ayew kutokana na kuwa majeruhi.
Habari zilizopatikana hii leo imemkariri kocha
huyo akisema amefikia uamuzi wa kumwacha mchezaji huyo baada ya kushindwa
kujiunga na wenzake kambini huko Abu Dhabi kufuatia kutopona jeraha la misuli
ya paja.
Mwisho wa kutaja vikosi
kwa nchi zitakazoshiriki fainali za kombe la mataifa ya Afrika mwaka huu ni january 9 na kutokana na
Ayew anayeichezea Marseille ya Ufaransa kushindwa kupona vyema inamfanya
ashindwe kujumuishwa kikosini.
Fainali za kombe la
mataifa ya Afrika zinataraji kuanza januari 19 nchini Afrika Kusini na kufikia
tamati yake mwezi february.
0 comments:
Post a Comment