Klabu ya soka ya Newcastle United
inayoshiriki ligi kuu ya England imethibitisha kumsajili aliyekuwa mchezaji wa
timu ya Montpellier ya Ufaransa Mapou
Yanga-Mbiwa kwa mkataba wa miaka mitano na nusu.
Yanga-Mbiwa ambaye alikuwa nahodha wa Montpellier amekabidhiwa
jezi namba 13 na anatarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza akiwa na Newcastle
United jumanne ijayo dhidi ya Aston Villa.
Akizungumza mara baada ya kuthibitishwa rasmi kuwa mchezaji wa Newcastle United Yanga-Mbiwa amesema anajisikia faraja kuitumikia timu hiyo huku kocha Alan Pardew akisifu kipaji kikubwa alichonacho nyota huyo.
Uongozi wa Montpellier jana ulithibitisha kufikia makubaliano na
Newcastle United juu ya uhamisho wa raia huyo wa Ufaransa ambaye ameripotiwa kufaulu vipimo vya afya na
kukubaliana mambo binafsi na timu yake mpya.
0 comments:
Post a Comment