Kamati ya kombe la Muungano ipo katika mikakati ya
kujaza nafasi za uongozi wa kamati hiyo ikiwemo nafasi ya mwenyekiti iliyoachwa
na mbunge wa zamani wa Mufindi Marehemu Benito Malangalila.
Mratibu wa mashindano hayo, Daudi Yassin amesema
kukamilika kwa zoezi hilo litakalo chukua wiki mbili kutoka sasa litafanikisha zoezi
la uandaaji wa michuano hiyo kwa mwaka huu.
Msimu uliopita michuano ya Muungano haikufanyika
kutokana na kuchelewa kwa ukamilifu wa mipango ya udhamini unaofanikisha
michuano hiyo kufanyika bara na visiwani.
0 comments:
Post a Comment