Uongozi
wa timu ya Njombe Mji toka mkoa mpya wa Njombe umedhamiria kuutangaza mkoa huo
kwa kutinga ligi kuu ya Tanzania bara kabla ya mwaka 2015.
Katibu
wa Njombe mji Kaini Nyigu amesema hayo jioni ya jana baada ya kumaliza mchezo
wa ligi ya mkoa dhidi ya Polisi Ludewa uliomalizika kwa timu ya Njombe mji
kushinda magoli 8 kwa 2.
Kaini
amesema mafanikio hayo yametokana na
maandalizi mazuri kabla ua kuanza kwa ligi ambapo walijihimu kucheza michezo
mingi ikiwemo na timu ya taifa ya vijana Serengeti boys kwa lengo kujiimarisha
zaidi.
Aliongeza
kuwa lengo la klabu yao kurejesha heshima ya soka la nyanda za juu kusini
iliyopotezwa na baadhi ya vilabu vikiwemo Lipuli, Tukuyu Stars pamoja na
Nazaret ya Njombe.
Mwaka
uliopita klabu hiyo ilishindwa kufanya vema wakati ikishiriki ligi kama klabu
ya mkoa wa Iringa kitendo ambacho kaini amedai kushindwa kwao kumechangiwa na
mizengwe ya uongozi wa soka mkoani Iringa.
0 comments:
Post a Comment