WADAU WAANZA KUINGA MKONI LIPULI.



Siku chache baada ya uongozi wa Lipuli kupitia mwenyekiti wakae Abnery Mrema kutangaza nia ya kuipandisha timu hiyo kongwe ya mkoa wa Iringa kwa kuunda kamati ya fedha huku akiwataka wadau kujitokeza kuichangia timu hiyo, mdau wa michezo ambayo pia ni mumbe wa NEC wa chama cha mapinduzi Mh. Muimage Madenge ametanga kuiopanguvu timu hiyo yenye maskani yake wilaya ya Iringa mjini.
Madenge amesema katika hatua yake ya kwanza atatoa kiasi cha shilingi laki tano atakayokabidhi siku ya jumatatu ili kufananikisha mipango ya awali ya klabu hiyo, huku akisisitiza kuwa ni wakati muafaka kwa wadau wa soka Iringa kutazama timu hiyo iliyobeba jina kubwa lenye heshima duniani.
Siku moja iliyipita mwenyekiti wa Lipuli Abnery Mrema alitangaza safu ya watu nane watakao simama katika kamati ya uhamasishaji wa timu hiyo. Huku kamati hiyo ikiongozwa na mheshimiwa Rita Kabati kama mwenyekiti wa kamati, Mhe, Ali Mbata katibu wa kamati  huku wajumbe wakiwa ni Fredirick Mwakalebela, Agostino Mrema,Haji Mwilu, Mohammed Msomali, Chuki Shabani pamoja na Husna Mtasiwa.
Mrema amesisitiza kuwa walioteuliwa kwenye kamati hiyo wamerdhia kuifanya kazi hiyo sambamba na kukubaliana na mkakati wa kupandisha katika ligi kuu bara timu ya lipuli ifikapo mwaka 2015.

0 comments:

Post a Comment