AZAM BINGWA KOMBE LA MAPINDUZI.



Fainali ya kombe la Mapinduzi imepigwa jana kwenye uwanja wa Amani kule Zanzibar ambapo timu ya Azam imetwaa ubingwa wa michuano hiyo baada ya kupata ushindi wa magoli 2 kwa 1 dhidi ya Tusker ya kenya.
Katika mchezo huo Tusker ilikuwa ya kwanza kufunga katika dakika ya 59 kupitia mshambuliaji wake Jese Were, wakati magoli ya Azam yakifungwa na  Jockins Atudo  kwa mkwaju wa Penati dakika 72 na Gaudience Mwaikimba 92.
Meneja wa Azam FC, Patrick Kahemele amesema ushindi huo umeletwa na kujituma kwa wachezaji wa klabu hiyo kuliko wapelekea kutoka kwenye kichapo cha goli moja hadi kushinda magoli 2 kwa 1.
Kwa matokeo hayo Azam imefikia rekodi ya Yanga ya mwaka 2004 na 2005 kwa kutwaa taji hilo na kulitetea.
Kwa upande mwingine Kahemelea amesema kuwa kikosi cha Azama kitasafiri mwishoni mwa juma hili kuelekea Kenya kwaaajili ya michezo ya kirafiki ambayo ni sehemu ya maandalizi ya ligi kuu na michezo ya kimataifa.

0 comments:

Post a Comment