
Siku
moja kabla ya kesho jumapili kucheza mchezo wa FA Cup dhidi ya Swansea kule
Libery Stadium, Meneja wa klabu ya Arsenal Arsene Venga amekiri kuchanganyikiwa
juu ya kukosa mataji akiwa na klabu yake ya Arsenal kwa miaka takribani nane
sasa.
Venga
amesema hayo wakati akizungumzia maandalizi ya mchezo wa raundi ya tatu ya
michuano ya FA Cup dhidi ya Swansea ambapo amekiri kuona ukame wa mataji unaoendelea
kwenye kikosi chake huku wakitazama vilabu vingine vikitwaa mataji tofauti.
Mfaransa
huyo amesema anafikiri kuwa Arsenal ipo kwenye mwendo mzuri ila kiti kitakacho
imarisha kikosi chake vizuri zaidi ni kutwaa taji la FA Cup ili kujenga imani
ya washabiki kwenye klabu hiyo.
Desemba
mwaka jana Arsenal iliondolewa kwenye robo fainali ya Capital One baada ya
kufungwa na Bradford kwa mikwaju ya penati lakini sasa Wenger ameonesha nia ya
kutaka kuindoa Swansea ambayo tayari iliifunga Arsenal magoli 2 kwa 0 kwenye
mchezo wa ligi kuu ya England.
Huu
ni mwaka wa nane sasa Arsenal haijafanikiwa kutwaa kombe lolote huku mara ya
mwisho Arsenal kufanya hivyo ni mwaka 2004 ilipotwaa taji la ligi kuu ya Englnd
bila ya kufungwa hata mchezo mmoja.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment