MAKINDA ATAKIWA KUTAZAMA NGUMI ZA NYUMBANI.




Spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anna Makinda, ameombwa kuwasaidia mabondia wa mkoa wa Njombe kwa lengo la kuinua mchezo wa ngumi katika mkoa huo mpya.
Hayo yamesemwa na raisi wa Oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yasini Abdalaha Ustadh wakati akizungumza juu ya uwezo wa bondia wa Njombe Chupak Chipindi.
 Ustadh amesema si vizuri kwa mkoa wa Njombe ambao umetoa muheshimiwa na spika wa bunge la Tanzania lakini hakuna mchango wowote juu ya wanamasumbwi wa mkoa huo hukua akisisitia kuwa fursa kubwa ya kuinua mchezo wa ngumi mkoani humo ipo kwa Spika wa Bunge kwa sasa anapaswa kutazama zaidi mabondia wa mkoa huo.
Akimzungumzia Chupak Chipindi amesema Chupak ni bondia bora na anahitaji kupata wawezeshaji ili kuweza kutangaza kipaji chake na autangaze mkoa wa Njombe,
Chupak ni bondia wa uzito wa juu alikuwa akiwakilisha mkoa wa Iringa hapo zamani kwa sasa Njombe mwishoni mwa mwaka 2012 alishindwa kwenda nchini Hungary katika pambano la kimataifa huku moja vikwazo vilielezwa kuwa ni ukata wa fedha.

0 comments:

Post a Comment