
Badaa ya kamati ya utendaji ya TFF,kukaa Novemba 3 mwaka huu
yaliyopokelewa na kamati hiyo taarifa ya mapendekezo ya marekebisho ya Katiba
TFF kama ifuatavyo:
1. Kuingiza kipengele
kinachohusu “Club Lincencing” kama ilivyoagizwa na CAF katika waraka wake
unaowataka wanachama wote wa CAF, ikiwemo TFF, kuhakikisha kuwa kipengele hicho
kinaingizwa katika katiba zao.
2. Kutokana na ushauri
na maagizo ya FIFA, TFF inatakiwa kuunda wa Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi
(“Elections Appeals Committee”) na kuondokana na utaratibu tulionao hivi sasa
ambao Kamati ya Rufaa (“Appeals Committee”) inajigeuza na kuwa Kamati ya Rufaa
ya Uchaguzi wakati wa mchakato wa uchaguzi wa TFF.
3. Kuindoa nafasi ya
Makamu wa Pili wa TFF pamoja na kutamka kuwa Wawakilishi wa klabu za Ligi Kuu
katika Kamati ya Utendaji watachaguliwa moja kwa moja na klabu zenyewe. Hii
inatokana na azimio la Mkutano Mkuu uliopita la kuruhusu uundwaji wa chombo
huru cha kusimamia Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza pamoja na kupitishwa kwa
Kanuni zinazokiongoza chombo hicho kama zilivyopendekezwa na klabu za Ligi Kuu
na kupitishwa na Kamati ya Utendaji.
Baada ya kutafakari mapendekezo hayo, Kamati ya Utendaji ya
TFF iliamua kuwa:
1. Ipo haja ya kuifanyia
marekebisho Katiba ya TFF kama iliyopendekezwa.
2. Kwa vile mapendekezo
mawili kati ya matatu ya marekebisho ya Katiba yana uhusiano na Uchaguzi Mkuu
wa TFF, ipo haja ya marekebisho hayo kufanyika kabla ya kutangazwa kwa Mkutano
Mkuu wa TFF na kuanza kwa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa TFF.
3. Aidha, kwa vile TFF
haina uwezo wa kuitisha mikutano mikuu miwili – Mkutano Mkuu Maalum kwa ajili
ya marekebisho ya Katiba ya TFF; na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi – katika kipindi
kifupi kijacho, marekebisho ya Katiba yafanywe kwa njia ya Waraka (“Circular
Resolution”).
0 comments:
Post a Comment