Mpaka aitaka wizara ya fedha kutazama timu za mikoa.



RAS wa mkoa wa Iringa, Mheshimiwa Getrude Mpaka, ameitaka wizara ya fedha kuzitazama timu za mikoa na idara mbalimbali za serikali katika kuziwezesha kifedha ilikuziweka katika hali nzuri kimashindano kama zilivyo timu za wizara mbalimbali.
Mpaka amesema hayo katika hafla fupi ya kukabidhiwa zawadi ya mshindi wa pili iliyoletwa na timu ya kuvuta Kamba kwa wanawake toka mkoani Iringa.
Katika hafla hiyo iliyofanyika ofisini kwake Mpaka amesema ni dhahiri kwamba wanashindwa kushiriki michezo mingi katika michuano ya Shimiwi kutokana na uhaba wa fedha za maandalizi na tofauti na timu za wizara ya fedha na nyinginezo wana mudu kushiriki takribani michezo yote kutokana na kuwa na fedha za kutosha za maandalizi.
Kwa upande mwingine Mpaka amewataka wanamichezo hao wa Serikali ya mkoa wa Iringa kufanya mazoezi kila kukicha ili kuboresha vikosi vyao kwaajili ya michuano mbalimbali.
Naye nadhoa wa timu ya kuvuta Kamba mkoani humo Agness Mlula amemshukuru Mh.Mpaka kwa ushirikiano alioutoa hadi kufikia mafanikio huku akisisitiza juu ya serikali kuu kuziangalia timu hizo ziweze kufanya vema kwenye michezo.
Michuano ya SHIMIWI kwa mwaka 2012 ilifanyika mkoani Morogoro ambapo ilianza  Sepetemba 22 na kumalizika Oktoba 6  huku timu ya Ras Iringa ikitoka na zawadi ya kikombe baada ya kuvutwa na timu ya Ikulu waliyokutana nayo kwenye mchezo wa fainali.

0 comments:

Post a Comment