
Rais wa CAF Issa Hayatou.
Baraza la vyama vya Soka Afrika mashariki CECAFA na
shirikisho la soka la nchini Uganda nd FUFA alimethibitisha kuwa raisi wa CAF
Issa Hayatou atakuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya ufunguzi wa michuano ya CECAFA
Challenge Cup inayotaraji kuanza hivi karibu Novemba 24 mwaka kule nchini
Uganda.
Akithibitisha hilo msemaji wa FUFA na CECAFA Rodgers Mulindwa
amesema tayari mipango imekalika na Hayatou atawasili nchini Uganda Novemba 22
na kuhudhuria kwenye haflaya ufunguzi huku akipokewa na raisi wa CECAFA Leodga
Chila Tenga.
Kwa upande wake raisi wa FUFA Lawrence Mulindwa amesema ni
heshima kubwa kwa Uganda kuandaa michuano hiyo lakini pia ni nguvu ya kutosha
katika kukuza endapo Hayatou atashiriki kwenye michuano hiyo mikubwa ya
ukandahuu wa CECAFA..
Katika michuano hiyo Novemba 24 Uganda itafungua dimba na Kenya
kwenye mchezo mkubwa Ufunguzi wakati Tanzania bara itacheza Nove 25 na Sudan.
0 comments:
Post a Comment