Mchungaji Msigwa aongeza nguvu kwenye soka la Iringa.



    
Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mch. Peter Msigwa ameandaa michuano mikubwa wilayani humo itakayoshirikisha takribani vilabu 28 vya jimboni mwake.
Akizungumza na blog hii, mratibu wa michezo kwenye ofisi ya mbunge huyo Abu Changawa amesema michuano hiyo itakayochezwa kwa mtindo wa makundi ambayo yatatoka kila kanda ya jimbo hilo inataraji kuanza Nov 26 mwaka huu na  imegharimu kiasi cha shilingi milion kumi na nane na laki tano za kitanzania (18,500,000/=) kwa maandalizi ya vitu vyote vya mashindano mpaka zawadi za michuano hiyo.
Changawa amesema kabla ya kuanza kwa michuano hiyo kilatimu itapewa jezi kwaajili ya maandalizi ya kushiriki michuano hiyo, na kwa upande wa zawadi  bingwa michuano hiyo atapa kitita cha shilingi milioni moja, mshindi wa pili shilingi laki saba wakati mshindi wa tatu atachukua kiasi cha shili laki tano, mbali na zawadi hizo kutakuwa na zawadi za timu yenye nidhamu, mfungaji bora, kipa bora pamoja na mwamuzi bora ambao wote watapata zawadi ya shilingi laki moja moja.
Wakati huo huuo Mch. Msigwa hakuwasahau waandishi wa michezo baada ya kutenga zawadi ya shilingi laki tatu kwa mwandishi bora wa gazeti, redio, na TV  wakati mshindi wa pili  tasnia hii ya habari wakipangwa kuchukua kiasi cha shilingi mbili kwa kila Nyanja.
Mwanzoni mwa mwezi uliopita Mheshimiwa Mch. Msigwa alikilaumu chama cha soka cha wilaya ya Iringa mjini IMDFA kwa kumnyima nafasi ya kudhamini ligi ya wilaya hiyo kwa madai kuwa wameiingiza siasakwenye mchezo wa soka na sasa ligi hiyo inadhaminiwa na Fredilick Mwakalebela.

0 comments:

Post a Comment