Chama cha
soka wilayani Mufindi umeongeza siku moja ya kukusanya fomu za usajili wa
vilabu vilivyoshindwa kufikisha fomu za
usajili wa wachezaji kwa wakati katika ofisi za chama hicho.
Katibu wa
MUDIFA Festor Kilipamwambu amesema tarehe ya mwisho ya kurejesha fomu hizo ni leo
lakini mpaka sasa vilabu 12 vimerejesha na takribani vilabu vitano havija
rejesha fomu hizo ndio maana wamefikia maamuzi ya kuongeza siku hadi Novemba 21 kwaajili ya kurejesha fomu hizo.
kwa upande mwingine Kilipamwambu amesema kuwa siku ya Alhmisi watakuwa na kikao na viongozi wote wa vilabu ili kuzungumzia mustakbali wa ligi na ratiba ya ligi hiyo.
0 comments:
Post a Comment